Jumamosi 24 Mei 2025 - 20:22
Njia yenye Athari kwa ajili ya Kupokelewa Dua

Hawza/ Katika kitabu "Bahjat al-Du‘a", pameelezwa ushauri wenye athari kubwa kutoka kwa Ayatollah Bahjat kuhusiana na kupokelewa dua.

Shirika la Habari la Hawza – Ushauri wa Ayatollah Bahjat (ra) kuhusu kupokelewa dua ni huu:

"Mojawapo ya njia ya kisheria kwa ajili ya kupokelewa dua na kukidhiwa haja ni kwamba: Mtu mwenye haja au mwenye matatizo aombe dua na amuombe Mwenyezi Mungu ayaondoe matatizo yote yanayofanana na matatizo yake kutoka kwa Waumini wa kiume na wa kike wote walio na matatizo hayo; au atimizwe haja yoyote inayofanana na haja yake kwa waumini wote; kwani katika hali hiyo, malaika humuombea dua yeye binafsi, na dua ya malaika huwa inakubaliwa."

Lebo

Maoni yako

You are replying to: .
captcha